WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka wajumbe wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Katavi kuweka ratiba ya kukagua ujenzi wa barabara na madaraja badala ya kusubiri kuletewa taarifa na watendaji.
Amesema hayo leo mchana (Alhamisi, Agosti 30, 2012) wakati akizungumza na wajumbe wa Bodi hiyo kwenye mkutano wa kwanza wa Bodi hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa Idara ya Maji mjini Mpanda. Waziri Mkuu aliizindua rasmi Bodi hiyo leo.
“Si vibaya mkiamua kuipa Bodi hii ratiba na mkaamua kwenda kuona hali halisi ya ujenzi wa barabara na madaraja au makalavati badala ya kusubiri kuletewa taarifa na watendaji wa idara,” alisema.
Alisema kuna umuhimu wa kujiwekea mazoea ya kwenda kuangalia barabara au madaraja wakati zinajengwa ili kujiridhisha na kiwango cha kazi kinachofanyika pale. “Unaweza usiwe mtaalam wa ujenzi lakini kama kazi ni mbovu si utaiona, si utapata nafasi ya kuhoji kulikoni au kuarifu mamlaka husika?” aliongeza.
Alisema katika mwaka wa fedha 2011/2012 (wakati huo mkoa huu ukiwa ni Wilaya ya Mpanda) zilitolewa sh. bilioni 5.5/- ambazo zimetumika kujenga barabara kwa viwango tofauti vyenye jumla ya kilometa 1,186.62 na madaraja ama makalvati makubwa 52.
Katika kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa sh. bilioni 10.65/- ambazo zimepangwa kujenga barabara kwa viwango tofauti zenye urefu wa kilometa 1,310.06 na madaraja pamoja na makalvati makubwa 58.
inapatikana fullshangwe.blogspot.com
Amesema hayo leo mchana (Alhamisi, Agosti 30, 2012) wakati akizungumza na wajumbe wa Bodi hiyo kwenye mkutano wa kwanza wa Bodi hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa Idara ya Maji mjini Mpanda. Waziri Mkuu aliizindua rasmi Bodi hiyo leo.
“Si vibaya mkiamua kuipa Bodi hii ratiba na mkaamua kwenda kuona hali halisi ya ujenzi wa barabara na madaraja au makalavati badala ya kusubiri kuletewa taarifa na watendaji wa idara,” alisema.
Alisema kuna umuhimu wa kujiwekea mazoea ya kwenda kuangalia barabara au madaraja wakati zinajengwa ili kujiridhisha na kiwango cha kazi kinachofanyika pale. “Unaweza usiwe mtaalam wa ujenzi lakini kama kazi ni mbovu si utaiona, si utapata nafasi ya kuhoji kulikoni au kuarifu mamlaka husika?” aliongeza.
Alisema katika mwaka wa fedha 2011/2012 (wakati huo mkoa huu ukiwa ni Wilaya ya Mpanda) zilitolewa sh. bilioni 5.5/- ambazo zimetumika kujenga barabara kwa viwango tofauti vyenye jumla ya kilometa 1,186.62 na madaraja ama makalvati makubwa 52.
Katika kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa sh. bilioni 10.65/- ambazo zimepangwa kujenga barabara kwa viwango tofauti zenye urefu wa kilometa 1,310.06 na madaraja pamoja na makalvati makubwa 58.
Post a Comment