. :
Home » » SAMATTA: GOLI LANGU DHIDI YA CAMEROON NI OMBI LANGU LA MSAMAHA KWA WASHABIKI NA NAAMINI WAMENISAMEHE

SAMATTA: GOLI LANGU DHIDI YA CAMEROON NI OMBI LANGU LA MSAMAHA KWA WASHABIKI NA NAAMINI WAMENISAMEHE

Written By KITUMBO GALAXY on Friday, February 8, 2013 | 6:39 AM

MBWANA Samatta amesema kuwa anaamini goli la ushindi alilofunga dhidi ya Cameroon linatosha kumsafisha kwa mashabiki wake.
 

Hiyo imekuja baada ya mashabiki wa soka kuwazomea pamoja na Thomas Ulimwengu wakati Stars ikicheza na Zambia, mwaka jana kwenye uwanja wa Taifa.
 

Nikutokana na kuchelewa kuripoti kambini kujiwinda na mchezo huo wa kirafiki na Chipolopolo mwakajana.
 

Kitendo hicho kilimkasirisha kocha Kim Poulsen ambaye aligoma kuwapanga kwenye kikosi ambacho kilicheza mtanange huo.
 

Stars iliibuka na ushindi wa bao 1-0. Bao hilo pekee, likizamishwa na Mrisho Ngassa kwa shuti la mwendo mrefu.
 

"Naamini ushindi huu utakuwa umewafurahisha mashabiki na kurudisha imani kwetu." alisema Samatta.
 

Alisema haikuwa lengo leo kuchelewa kujiunga na kambi ya timu isipokuwa ni mambo tu yaliingiliana.
Ahsante sana shafii dauda
Share this post :

Post a Comment

 
Support : Kitumbo | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. KITUMBO GALAXY - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger